KUZUIA UGONJWA WA FIGO
Ugonjwa wa figo ni ugonjwa unaoathiri figo hatua
kwa hatua na hatimae husababisha figo kufeli au kushindwa kufanya kazi vizuri,
wakati huu wa ugonjwa wa figo unapofikia hatua ya juu kabisa basi majimaji
hatarishi na takamwili hujijenga katika mwili,na hii yote ni kwa sababu figo
inakazi nyingi sana katika mwili wa binadamu na mojawapo ni;
Kuchuja
uchafu kwenye damu na kutoka nje kama mkojo, kazi nyingine ya figo ni kuachilia
vichocheo mbalimbali mwilini ili mwili ufanye kazi vizuri kama vile, kemikali
aina ya renini hii husaidia mwili ili usiwe na tatizo la kuwa na ugonjwa wa
shinikizo la damu maarufu kama presha, lakini pia huachilia kemikali ambao kazi
yake mwili ni kuhakikisha chembe chembe hai nyeupe na nyekundu zinakuwepo za
kutosha ili kuepusa upungufu wa damu kwenye mwili, hivyo basi kuna maradhi
mengi yanasababisha fingo kushindwa kufanya kazi vizuri baadhi ya magonjwa hayo
ni; ukimwi,kisukari, pressure,chujio la mkojo kushambuliwa na wadudu kama vile
wadudu wa UTI, figo kuwa na mawe (kidney stone) na saratani ya figo.
UTAGUDUAJE KUWA FIGO YAKO IMESHAAZA KUATHIRIKA.
Kuna
dalili nyingi sana ambacho unaweza kuziona kama figo imeshaaza kuwa na matatizo
mbalimbali katika mwili na leo tutajifunza dalili za haraka kuziona na kutambua
kuwa figo inaashiria kupata tatizo au tayari ishakuwa na tatizo nazo ni;
·
Kukosa hamu ya kula na kukosa radha ya
kinywani, mara nyingi sana mtu anapokuwa na changamoto ya figo kushidwa kufanya
kazi humpelekea kukosa hamu ya kula na kujiona kuwa ameshiba na haitaji kula
kabisa hii husababishwa na kutokuachiriwa kwa kemikali zinazomfanya mtu ajihisi
kuwa anahitaji kula au kupata chakula
·
Kubadirika kwa rangi ya mkojo. Hii siyo kwamba
ni kiashiria cha moja kwa moja bali muda mwingine inaweza ikaonyesha kuwa
haupati maji ya kutosha mwilini mwako, na mkojo unatakiwa uwe wa rangi nyeupe
hivyo mtu alie na changamoto ya figo anaweza kuwa na mkojo wajano,mwekundu kama
damu na unakuwa na harufu kali sana.
·
Maumivu ya mgogo, kiuno,na joints.
·
Kushidwa kupumua vizuri, hii ni kwa sababu
kunakuwa hamna uwiano wa damu na maji mwilini ili kuufanya mwili uwe kwenye
msawazo mzuri wa ufanyaji kazi.
·
Kushindwa kulala vizuri na muda mwigine
humfanya mtu kushidwa kugeuza hata shingo japo dalili hii inaweza kuwa ni ya
moja kwa moja au sababu nyingine
·
Miguu kuvimba au kuwaka moto
·
Kuona giza na kizunguzungu
·
Kuishiwa au kupotea kwa uwezo wa
tendo la ndoa au nguvu za kiume
Lakini
ndugu mfuatiliaji wa nakala zetu za nutrijoju global health tambua kuwa
matibabu ya figo watu wengi hushidwa kumudu gharama zake na kadiri
unavyochelewa kujiimarisha punde uonapo dalili kama hizo husababisha maafa/kifo yasiyo ya lazima na maadiko yanasema watu
wanaagamia kwa kukosa maarifa.
NINI
KIFANYIKE ILI KUTUNZA FIGO.
Kuna
sababu nyingi zinazosababisha figo kuharibika navyo ni, unywaji wa Pombe kupita
kiasi hii inapelekea figo kushidwa kutenganisha takamwili vizuri ili zitolewe
nje kwa sababu ya sumu nyingi iliyomo kwenye kinywaji aina ya pombe,
kutokufanya mazoezi unapofanya mazoezi mwili unaupa nafasi ya kuhakikisha
utoaji wa sumu kupitia milango ya fahamu uko vizuri mtu unapokuwa hufanyi
mazoezi ni kiepesi kuharibu figo kwa sababu ya sumu, uzito mkubwa kiafya mtu
anatakiwa awe na uzito ulio sawa na urefu wake BMI kwani uzito mkubwa na mara
nyingi ndo chanzo kikuu cha kusababisha ugonjwa pressure ya kupanda na hapo juu
tumeongelea kuwa presha inaathirije figo.
SULUHISHO
KWA MTU ALIE NA CHANGAMOTO YA FIGO
Utumiaji wa virutubisho/supplement ni muhimu
sana ili kuweza kurudisha ubora wa mwili na afya kwa ujumla, tatizo la figo ni
tatizo ambalo kama mtu hutaweza kuwahi kuimarisha hata kupoteza uhai ni kugusa
tu hivyo kuna bidhaa ambazo zinasaidia kujenga figo vizuri hata ikiwa imeshaaza
kureta shida, kuondoa sumu mwilini ,kuondoa mawe yaliyoadhiri figo, kuimarisha
kam tayari figo imeanza kufeli na hivyo utapata msaada wa kuelimishwa ule
vyakula kuligana na kundi lako la damu ili kurudisha uwezo wa mwili wako
vizuri,
Unaweza
kuwasiliana na kampuni moja kwa moja kupata elimu kwa upana Zaidi.


1 Comentarios
Nakubal sana ushauri wako.ila km kiuno kinauma tatizo linakuwa ni nn
ReplyDelete